Image
Image

Rais Kikwete: Shutuma dhidi ya Tanzania DRC ni za kudharauliwa



Tanzania imesema kuwa ni jambo la kusadikika na kufikirika tu kwa baadhi ya watu kudai kuwa haiko tayari kukabiliana na vikundi vya uasi na ugaidi (negative forces) vilivyobakia vikivuruga amani na kusababisha ukosefu wa utulivu ndani ya nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Badala yake, Tanzania inaendelea kuwa tayari kukabiliana na vikundi hivyo, kwa mujibu wa mamlaka ambayo majeshi yake pamoja na yale ya Afrika Kusini na Malawi, yamepewa na Umoja wa Mataifa (UN) ya kuvishambulia, kuvimaliza nguvu na kuvinyang’anya silaha (neutralize and disarm all negative forces) vikundi hivyo vyote.
Nchi hizo tatu zinaunda Brigedi ya Kimataifa ya Force Intervention Brigade (FIB), ambayo ni sehemu ya Majeshi ya UN katika DRC ya United Nations Stabilisation Mission in Congo (MONUSCO), yaliyoko chini ya Luteni Jenerali Alberto Santacruz wa Brazil. Chini ya mamlaka ambayo Brigedi hiyo imepewa na UN, majeshi ya nchi hizo tatu, yana uhalali wa kuvishambulia vikundi vya kiasi katika DRC.  
Msimamo huo wa Tanzania umerudiwa tena na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Januari 13, 2015, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Novisise Mapisa-Nqakula, Mjumbe Maalum wa Rais wa Afrika Kusini na Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo. Waziri Nqakula amefuatana na Waziri wa Usalama wa Afrika Kusini, Mheshimiwa Mahlobo.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wakati akiwatakia mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Tanzania Heri ya Mwaka Mpya wakati wa Halfa ya Mwaka ya Sherry Party iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Rais Kikwete aliyaeleza maoni na shutuma dhidi ya Tanzania kuwa ni mambo ya “kudharauliwa”.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Zanzibar, Rais Kikwete amemwambia Bibi Nqakula kuwa msimamo wa Tanzania umekuwa ule ule wa siku zote bila mabadiliko yoyote – yaani kuhakikisha kuwa majeshi na vikundi vyote vya uasi ndani ya DRC vinamalizwa. Rais Kikwete amekuwa Zanzibar tokea jana, Jumatatu, Januari 12, 2015 wakati alipohudhuria sherehe za miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Bofya Kujua zaidihttp://www.ikulu.go.tz/index.php/media/press_details/1273
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment