Image
Image

Umoja wa Afrika walaani vikali mashambulizi ya Boko Haram



Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bi Nkosazana Dlamini Zuma amelaani vikali mashambulizi yanayoendelea kufanywa na kundi la kigaidi la Boko Haram katika maeneo mbalimbali nchini Nigeria na sehemu nyingine za Afrika.


Kwenye taarifa yake, Bi Zuma ameeleza kushtushwa kwake na mauaji ya hivi karibuni katika soko la Potiskum kwenye mji wa Baga jimboni Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria. 

Shambulizi hilo linadaiwa kufanywa na washambulizi wawili wa kike wa kujitoa mhanga, huku mmoja akisemekana kuwa na umri wa miaka 10.

 Bi Zuma ametoa salamu za rambi rambi kwa familia za wahanga na kusisitiza kuwa, Umoja huo unasimama na watu pamoja na serikali ya Nigeria katika wakati huu mgumu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment