Mchezaji huyo wa taifa la Togo mwenye umri wa miaka 31
ameandika kuhusu matatizo ya familia yake katika mtandao wa facebook na kusema
kuwa alikuwa ameamua kujiua.
Adebayor Amekosa mechi ya jana jumapili kati ya
kilabu yake na Everton mbali na ziara ya Kuala Lumpur na baadaye nchini Sidney.
kocha wa kilabu hiyo Mauricio Pochettino amesema wamempa mda wa kusuluhisha
mzozo na familia yake. Amesisitiza kuwa hayo ni maisha yake binafsi. Amesema
aliongea naye mapema wiki iliyopita na kwamba hiyo ni hali ngumu kwake.
Adebayor alijiunga na klabu ya Spurs mwaka 2011 kutoka Manchester City kupitia
mkopo kabla ya mabao 18 aliyofunga akiwa na Hotspurs kumwezesha kupewa mkataba
wa kudumu.


0 comments:
Post a Comment