Kenya inapanga kuwapandisha kizimbani maofisa 29 wa
umma wanaokabiliwa na mashtaka mbalimbali ya ufisadi baada ya kutolewa
mapendekezo na Mkurugenzi wa Mwendesha Mashtaka wa Umma.
Afisa mkuu mtendaji wa Tume ya Maadili na Kupambana
na Ufisadi Halakhe Waqo amesema hadi sasa maofisa 19 wa umma wamefunguliwa
mashtaka baada ya kuanzishwa tena mapambano dhidi ya ufisadi miezi miwili
iliyopita.
Tume hiyo leo itawasilisha kwa Mwendesha Mashtaka wa
Umma nyaraka za mawaziri wanne waliosimamishwa kazi na rais mwezi Machi, ili
kutoa fursa ya kufanyika uchunguzi. Bw. Waqo amesema tume imekamilisha
uchunguzi wa nyaraka 56, ambapo 21 kati ya hizo zimeshapelekwa kwa Mwendesha
Mashtaka wa Umma. Tume imesema maofisa hao wa umma wataondolewa mashtaka baada
ya madai dhidi yao kuchunguzwa na kuonekana hawana makosa.


0 comments:
Post a Comment