Image
Image

News Alert:Wananchi masikini wanashindwa kupata haki zao mahakamani kutokana na kukosa msaada wa Sheria.


Asilimia  kubwa  ya wananchi  masikini wanashindwa kupata haki zao mahakamani kutokana na  kukosa  msaada wa sheria jambo linalosababisha  wengi  wao  kujikuta  wakipewa  adhabu  kubwa  zisizolingana na makosa  yao na wengine  wakipoteza  mali na rasilimali  zao .
Hayo  yamesemwa na Mtendaji  Mkuu  wa Umoja wa Mawakili   wa  Afrika,Bwana  DONALD  DEA ,alipokuwa akizungumzia hatua ya raia  wawili  wa  Kenya   na mmoja wa Tanzania kuvifikisha  vyombo  vya dola vya Tanzania  kwenye  Mahakama ya  Afrika vikilalamikiwa  kwa  ukiukaji  wa  haki za binadamu .
Bwana  DEA   amesema kimsingi  wananchi  wa kawaida  wanaofikisha  mashauri  yao  mahakamani  ambayo  adhabu ya jambo  linalolalamikiwa  inazidi kifungo  cha  miaka  20  wanahitaji  kupata msada wa sheria.
Rais  wa  mahakama  hiyo , Jaji  AGUSTONO  RAMADHAN  amesema  pamoja  na  mahakama  hiyo  kuanza  kuwa  kimbilio  la  watu  wanaoona  kuwa  haki zao  zimekiukwa,inakabiliwa  na matatizo mengi ikiwemo ya uhaba wa fedha .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment