Image
Image

Mugabe: Afrika bado imezingirwa na ukoloni mamboleo.


Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema bara la Afrika lingali limezingirwa na ukoloni mambo leo pamoja na athari mbaya za utandawazi.
Katika taarifa kwa mnasaba wa Siku ya Afrika ambayo inaadhimishwa leo, Mugabe ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika amesema Waafrika wana jukumu nzito sana la kukabiliana na sera za wakoloni mambo leo ambao wanataka kuvuruga ustawi wa kiuchumi na kisiasa ambao umepatiakana barani Afrika tokea ukoloni usambaratishwe. 
Amesema Umoja wa Afrika umechukua hatua imara kiuchumi na kisiasa kwa lengo la kulinda mustakabali wa Afrika. 
Amesema Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limechukua hatua za kuleta amani na usalama katika bara hilo .
Mugabe amesema  muungano wa kiuchumi baina ya nchi za Afrika ni stratijia ya dharura katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani humo. 
Rais wa Zimbabwe amesema bara Afrika lina utajiri mkubwa wa madini na kilimo na iwapo utajiri huo utatumiwa ipasvyo maisha ya watu barani humo yataboreka kupitia kuangamizwa njaa, umasikini na maradhi. 
Huku akiashiria kuhusu wimbi la Waafrika wanaopoteza maisha wakivuka Bahari ya Mediterranea wakitafuta maisha bora Ulaya,Mugabe ametoa wito kwa viongozi wa Afrika kuchukua hatua ya kuondoa taswira mbaya ya Afrika.  
Mugabe amekumbusha kuwa Waafrika wanakimbilia nchi za Ulaya ambazo zimetajirika kutokana na uporaji wa rasilimali za bara Afrika.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment