Rais Zuma akiwahakikishia wageni kutoka nchi
mbalimbali za Afrika usalama wa kuishi na kufanya kazi nchini Afrika Kusini
amesema, wananchi wa Afrika Kusini na raia wa kigeni waliotoka nchi zingine za
Afrika kutafuta fursa nchini humo wamekuwa na mshikamano, na wanapaswa
kuendelea na umoja huo kwa amani. Zuma amesema Siku ya Afrika pia ni kumbukumbu
ya namna Afrika Kusini ilivyopokea msaada na mshikamano kutoka nchi zingine za
Afrika wakati wa mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi. Akiashiria
migogoro iliyopo katika nchi kadhaa za Kiafrika, Rais wa Afrika Kusini pia
amesisitiza kuhusu umuhimu wa matatizo ya Waafrika kutatuliwa na Waafrika
wenyewe.
Maadhimisho haya ni ya 52 tangu kuanzishwa kwa Umoja
wa Nchi Huru za Afrika OAU mwaka wa 1963.


0 comments:
Post a Comment