Katika taarifa yake, Bwana Ban amesema kila nchi
inayokumbwa na tatizo hilo inapaswa kuunda mkakati jumuishi wa kitaifa, ambao
utalenga kutokomeza fistula katika kipindi cha kizazi kimoja.
Aidha ameiomba jamii ya kimataifa kuongeza misaada
yake kwa nchi zenye mahitaji zaidi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la
Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu UNFPA, Babatunde Osotimehin, amesema licha ya
mafanikio yaliyopatikana, mathalan kwa wanawake 47,000 waliofanyiwa upasuaji wa
kuponesha fistula, bado juhudi zinahitajika ili kupeleka huduma za afya za
uzazi katika jamii duniani kote, kwani bado visa 50,000 hadi 100,000 vya
fistula vinatokea kila mwaka.


0 comments:
Post a Comment