Serikali imetangaza kushusha kuanzia tarehe mosi
mwezi julai mwaka huu viwango vya kodi ya ardhi na gharama za upimaji ili kutoa
nafasi kwa Watanzania wengi kuwa na ardhi iliyopimwa hali itakayonchangia
kuondoa migogoro iliyokithiri ya ardhi hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi WILLIAM LUKUVI katika kikao cha baraza kuu la wafanyakazi
wa wizara hiyo ambapo amekiri kuwa gharama za ardhi ni kubwa na mara zote
wananchi wa kawaida hawana uwezo wa kulipa na kuchangia kuwepo migogoro ya
ardhi isiyo ya lazima.
Katika mkutano huo Katibu Mkuu wa wizara ALPHAYO
KIDATA aliwataka watendaji wa ngazi zote wanohusika na masuala ya ardhi
kuzingatia weledi na miiko ya kazi kufuatia sekta ya ardhi kunyooshewa vidole
kwa utendaji mbovu kila kukicha.
Kwa upande wao washiriki wa baraza hilo wamekiri
migogoro mingi ya ardhi ambayo mingine inasababisha hata kuwepo matukio ya vifo
na umwagaji wa damu ambayo yanachangiwa na baadhi ya maofisa wa ardhi na
changamoto ambazo zimekuwa zikichangia migogoro ya ardhi.


0 comments:
Post a Comment