Image
Image

Bocco ‘Adebayor’, viwanja vingi vya soka nchini havina hadhi ya kuchezewa Ligi Kuu.


STRAIKA wa Azam na Taifa Stars, John Bocco ‘Adebayor’, ameviangalia viwanja vya soka nchini na kuona vingi havina hadhi ya kuchezwa Ligi Kuu na sasa anataka kuanzisha kampeni ya nchi nzima kuhakikisha viwanja vinaboreshwa ili kuwarahisishia kazi wachezaji wanapokuwa uwanjani.
Akizungumza na Mwanaspoti jana Ijumaa, Bocco alisema ni lazima ianzishwe kampeni ya kuboreshwa kwa viwanja na yeye yupo tayari kutumia hata fedha zake kwa nauli ili kuhamasisha jambo hilo.
“Ushauri wangu wa kwanza tunaomba tuanze kampeni ya kurekebisha viwanja vinavyotumiwa kwa mechi za Ligi Kuu Bara, mimi najitolea hata mikoani nitaenda kwa nauli yangu mkitaka nisaidieni kwa  hilo,” alisema Bocco.
Bocco alisema angependa kampeni hiyo ianze mapema kabla ya kuanza kwa ligi ya msimu ujao  ili mambo yawe mazuri kabla ya kugeukia matatizo mengine yanayokwanza soka la Tanzania.
“Lazima tuanze mapema hili jambo, tuna viwanja vichache kwa ajili ya Ligi Kuu, vingine havifai na vimekuwa vikiwakwaza wachezaji na timu kwa ujumla, TFF lazima iamke mapema,” alisema Bocco.
Aidha Bocco aliweka hadharani maoni yake sababu ya Taifa Stars kufanya vibaya kwa miaka mingi na kuwasononesha Watanzania, usome waraka wake katika ukurasa wa tano.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment