Kauli hiyo inatokanana habari kuwa, rais Benigno
Aquino wa Philippines jana alisema ndege za Philippines zitaendelea kufanya
doria katika sehemu yenye mvutano katika bahari ya Kusini, na China haipaswi
kunyanyasa nchi ndogo. Bibi Hua Chunying anasema,
"Nahisi baadhi ya watu wa Philipines wanapiga
kelele na kufanya uchokozi juu ya suala la bahari ya Kusini. China imeweka wazi
msimamo wake. Nataka kuwakumbusha watu wa Philipines kwamba, China haiwezi
kufanya ubabe dhidi ya nchi ndogo, lakini pia tunaona kuwa nchi hizo ndogo
hazipaswi kufanya uchokozi bila kusita na bila msingi wowote. Tunaitaka
Philipines iache vitendo hivyo, na kurudi kwenye njia ya mazungumzo ili kutatua
suala lililopo."


0 comments:
Post a Comment