Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa
Bernard Membe amesema hayo jijini Dar es Salaam jana usiku muda mfupi baada ya
kupokea taarifa ya hali ilivyo nchini Burundi kutoka kwa mawaziri wa Afrika
Mashariki waliopewa jukumu la kufuatilia mgogoro huo.
Kwa mujibu wa waziri Membe, hali ya nchini Burundi
imezidi kuwa tete kiasi cha kutishia usalama wa mataifa jirani na nchi hiyo na
kwamba juhudi za haraka zinahitajika katika kuutatua mgogoro huo.
Mbali ya marais wa nchi wanachama wa jumuiya ya
Afrika; viongozi wengine watakaohudhuria ni pamoja na Rais Jacob Zuma wa Afrika
Kusini, Jose Eduardo Dos Santos wa Angola, mwakilishi maalum wa katibu mkuu wa
Umoja wa Mataifa, mwakilishi wa kamisheni ya nchi za maziwa makuu, Kamishna wa
Umoja wa Afrika Bi. Nkosazana Zuma na wawakilishi wa vuguvugu la upinzani
nchini Burundi.


0 comments:
Post a Comment