Kikosi hicho kitaingia kambini mara baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo Hans Van de Pluijm kuwasili akitokea mapumziko.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja huyo alisema kuwa kwa sasa timu yao iko katika mapumziko baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Vodacom.
Alisema mazoezi hayo yatakuwa maalumu kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya kombe la Kagame yanayotarajiwa kuanza Julai, mwaka huu.
"Timu yetu itaingia kambini mapema ili kujiandaa na kombe la Kagame, kwani lengo letu ni kuhakikisha kombe linabaki nyumbani," alisema Hafidhi.


0 comments:
Post a Comment