Image
Image

Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu yatangazwa Ethiopia huku Chama tawala cha Ethiopia kikielekea kushinda kwa kishindo.

Chama tawala cha Ethiopia kinaelekea kushinda kwa kishindo uchaguzi mkuu wa nchi hiyo huku wapinzani wakilalamika kwa kudai kwamba wakati wa zoezi la kupiga kura wafuasi wao walinyanyaswa.

Uchaguzi huo ni wa kwanza tangu mwaka 2012 alipofariki waziri mkuu wa nchi hiyo Bwana Melesi Zenawi na kurithiwa na Bwana Hailemarian Desalegn.

Akizungumza baada ya kupiga kura kwenye jimbo lake la Gununo kilomita 330 magharibi ya mji mkuu wa nchi hiyo, Addis Ababa bwana Desalegn alisema hakukuwa na ukandamizaji wowote katika uchaguzi huo.

Chama tawala cha Ethiopia cha PEOPLE'S REVOLUTIONARY DEMOCRATIC FRONT EPDRDF kimejizolea sifa katika kukuza  uchumi wa nchi hiyo na katika bunge lililomalizika lililokuwa na wabunge 547 mbunge wa upinzani alikuwa  mmoja tu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment