Waziri mkuu wa zamani wa Israeli Bwana Ehud Olmert
amehukumiwa kifungo cha miezi minane jela kwa
kupatikana na hatia ya ubadhirifu na kukosa uaminifu.
Waziri mkuu aliyekuwa madarakani tangu mwaka 2006
hadi mwaka 2009 amepatikana na hatia ya kupokea fedha kutoka kwa mfuasi wake mmoja ambaye ni raia wa marekani wakati wa kusikilizwa kwa kesi
yake ya awali mwezi machi mwaka huu,kitu ambacho ni kinyume na katiba yao.
Adhabu hiyo ni mbali na kifungo kingine cha mwaka
jana ambapo alihukumiwa kifungo cha kwenda jela miaka sita kesi ya rushwa na
tayari amekata rufaa kupinga hukumu hiyo.



0 comments:
Post a Comment