Image
Image

News Alert: Kamati kuu ya CCM yafanya tathmini mwendendo wa zoezi la kura ya maoni*Yaitaka serikali kujadiliana na NEC ili kunusuru changamoto zinazo kabili zoezi hilo.


Kamati kuu CCM imefanya tathmini ya mwenendo wa mchakato zoezi la upigaji wa kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa na kuitaka serikali kujadiliana  na tume ya taifa ya uchaguzi  ili kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazolikabili zoezi hilo ambazo zinaweza kuwa kikwazo kwa kura hiyo kwenda sambamba na uchaguzi mkuu ujao kama ilivyotangazwa awali.

Kamati hiyo ambayo inalazimika kukaa kwa siku mbili mfululizo kinyume na ratiba iliyotolewa awali ya siku moja kinatoa ushauri huo baada ya kupitia hoja mbalimbali ambapo pamoja na mambo mengine imebaini zoezi la upigaji kura ya maoni ya katiba mpya linakbiliwa na changamoto lukuki zikiwemo kasi ndogo ya uandikishaji wa daftari la kudumu.

Changamoto zingine zilizobainishwa kuikabili kura hiyo ni pamoja na matakwa ya kisheria ambayo yanaelekeza zoezi hilo liende pamoja na utoaji wa elimu kwa wananchi kwa siku 60 siku 30 za kampeni na baada ya hapo ndipo ipegwe kura ya maoni ambapo tathmini inaonyesha hakutakuwepo na muda wa kutosha kabla ya tarehe 25 October inayotajwa kuwa ndio tarehe rasmi ya uchaguzi mkuu.

Katika hatua nyingine wakati macho na masikio ya watanzania yakielekezwa hapa Dodoma katika vikao vya juu vya CCM vinavyotajwa kuwa dira ya chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment