Mhanga wa kutoka kikundi cha wapiganaji cha dola la kiislamu amelipua bomu alilokuwa nalo katika msikiti kwenye jimbo la mashariki
nchini saudia arabia na kuua watu 21 na kujeruhi wengine 81.
Taarifa zinasema kuwa mhanga huyo alikuwa amevaa
bomu hilo ndani ya nguo zake na aliingia katika msikiti wa madhehebu ya Sunni
na kujifanya kama ameenda kuswali swala ya ijumaa ya kutekeleza unyama huo.
Mauaji hayo yanahusishwa na harakati za kikundi cha
dola ya kiislamu kupinga mashambulizi ya majeshi ya Saudia Arabia katika
nchi ya Yemen dhidi ya waasi wa kikundi
cha Houthi kinachoingoza kimabavu Yemen.


0 comments:
Post a Comment