Baada ya kukagua basi
hilo mkaguzi wa TFDA kanda ya mashariki Dokta. Ediga Mahundi amesema
walipata tarifa za siri kutoka kwa wasamaria wema ambapo waliweka mtego
katika mzani wa Kihonda mjini morogoro na kufanikiwa kukamata vipodozi hivyo.
Ameeleza kuwa vipodozi hivyo havifai kwa matumizi ya
binadamu na vimekuwa vikisababisha tatizo la watoto kuzaliwa na vichwa vikubwa na
hivyo kuwa na madhara.
Kwenye hali ya
kushangaza abiria waliokuwa wakisafiri
kwa basi hilo wameonekana kunywa maziwa yaliyokamatwa na mamlaka ya
chakula na dawa wakidai maziwa hayo ni salama kwa matumizi ya binadamu.
Hata hivyo wamezitaka mamlaka
husika kufanya ukaguzi wa vyombo vya usafiri kabla ya kuondoka na kuigia nchini
ili kubaini wale wote wanasafirisha bidhaa zisizo na ubora.




0 comments:
Post a Comment