Image
Image

Waandamanaji watatu wameuawa wakati polisi walipokuwa wakiwatawafanya waandamanaji katika mji wa Bujumbura nchini Burundi.


Waandamanaji  watatu wameuawa wakati polisi walipokuwa wakiwatawafanya waandamanaji katika mji  wa Bujumbura nchini Burundi ambao walikuwa wakipinga kitendo cha Rais Piere Nkurunzinza kugombea kiti cha urais kwa awamu ya tatu.

Waandamanaji  hao waliuawa baada ya jitihada za polisi wa nchini hiyo kuwataka watawanyike kawa amani kushindikana na pia kitendo cha polisi kufyatua risasi za moto hewani kuonekana kudharauliwa na wananchi hao na kisha polisi kuamua kuwafyatulia waandamanaji.

Kwingineko nchini huko baadhi ya watu ambao wamekamatwa na polisi kutokana na maandamano hayo imebainika kuwa ni watoto wadogo ambao walishiriki katika maandamano kuwaunga mkono wazazi pamoja na walezi wao kupinga kitendo cha rais Nkurunzinza kugombea kwa awamu ya tatu.

Inakaridiwa kuwa zaidi ya  raia wa burundi laki moja na ishirini wapo katika makambi ya wakimbizi katika nchi za Tanzania na Burundi ambapo wamekimbia  vurugu  baada ya chama cha CNDD -FDD kumpitisha rais Nkurunzinza kugombea kiti  hicho kwa awamu ya tatu kinyume na katiba inayomruhusu mtu kukaa madarakani kwa vipindi viwili tu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment