Mapigano hayo yametokea Tanhuato, jimbo la Michoacan
karibu na mpaka wa jimbo la Jalisco na polisi mmoja aliuawa kitendo
kilichoamsha ari kwa wapiganaji wa serikali .
Kamishna wa usalama wa taifa nchini humo Bwana Monte Alejandro Rubido amesema katika
mapigano hayo yaliyochukua saa tatu
idadi kubwa ya silaha pia zilikamatwa zikiwemo bunduki 30 za aina ya 'RIFLE'.
Kwa miaka kadhaa sasa serikali ya Mexico imekuwa ikipambana na makundi ya
wauzaji wa dawa za kulevya ambao wamejizatiti na kuwa na silaha kama ambazo
serikali inazimiliki.


0 comments:
Post a Comment