Image
Image

News Alert: Mbowe awaonya wagombea chadema*Asema chama hakiendi ikulu kulipiza kisasi.


Chama cha demokrasia na maendeleo kimewaonya makada wake ambao wanakusudia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi mkuu ujao kuwa wasijaribu kujihusisha na vitendo vya kutoa rushwa ili kushawishi wateuliwe kipitia Chadema,kwa kuwa  chama hicho hakitamteua mtu kwa kigezo cha fedha, kabila wa rangi yake bali kwa kuzingatia sifa na vigezo vilivyowekwa na chama.

Onyo hilo limetolewa wilayani Rungwe  na mwenyekiti wa taifa wa chama cha demokrasia na maendeleo, Chadema, Freeman Mbowe  wakati akizungumza na viongozi wa ngazi ya wilaya, majimbo na watu ambao wametangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kupitia chadema .

Katika hatua nyingine mbowe amesema kuwa chama chake kinapambana kushika dola sio kwa lengo la kwenda ikulu kulipiza kisasi,bali kinataka kushika madaraka ili kuwaletea watanzania neema ya maendeleo kwa kufanya mambo ambayo chama cha mapinduzi kimeshindwa kuwafanyia watanzania.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chadema mkoa wa mbeya, joseph mwachembe, maarufu kwa jina la china amelalamikia tume ya taifa ya uchaguzi, NEC, kwa kutowashirikisha wadau ipasavyo katika zoezi la uandikishaji wapigakura kwenye Daftari la kudumu kwa Teknolojia ya Biometric Voters Registration, BVR.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment