Image
Image

News alert:Hospitali ya rufaa ya mkoa wa mwanza Sekou Toure imepatiwa Kompyuta 25 zenye thamani ya shilingi milioni 30.


Hospitali ya rufaa ya mkoa wa mwanza Sekou Toure imepatiwa Kompyuta 25 zenye thamani ya shilingi milioni 30 ambazo zitatumika  kuhifadhi kumbukumbu za wagonjwa na kuboresha makusanyo ya fedha kwa njia za kielektroniki ili kwenda sambamba na mpango wa afya wa miaka mitano wa 2013 – 2018 unaolenga kuingiza huduma za afya katika mifumo ya kielektroniki.
Kompyuta hizo ambazo zinaambatana na huduma za bure za Internet isiyo na kikomo zimetolewa na kampuni ya Huawei Tanzania kwa ushirikiano na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo kwa lengo la kuijengea uwezo Hospitali ya Sekou Toure katika utunzaji wa kumbukumbu za afya, ambapo serikali kupitia kwa mkuu wa wilaya ya nyamagana Baraka Konisaga imetoa pongezi za dhati kwa makampuni hayo kutokana na michango yao mbalimbali kwa jamii.

Akiongea wakati wa kukabidhi msaada huo, meneja mkuu wa Tigo Diego Gutierrez amesema kwamba msaada uliotolewa kwa hospitali hiyo ya rufaa ni katika kutekeleza mkakati wa kampuni ya tigo wa kuyabadilisha maisha ya watanzania ili kuwa ya kidijitali katika maeneo yote, sekta ya afya ikiwa ni mojawapo, huku afisa mtendaji mkuu wa Huawei Zhang Yongquan akisema kwamba msaada huo unaonyesha jinsi ambavyo kampuni yake imejitolea kusaidia sekta ya afya ili iendane na mabadiliko ya kiteknolojia.

Mapema mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa mwanza Sekou Toure Dk. Onesmo Rwakyendela pamoja na mwenyekiti wa bodi ya Hospitali hiyo Christopher Mwita Gachuma wameshauri Kompyuta hizo zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa ili ziweze kudumu kwa muda mrefu, kwani matumizi mazuri ya kompyuta hizo yatawahamasisha wadau wengine wa maendeleo kuendelea kuwekeza misaada yao ya hali na mali katika hospitali hiyo yenye uwezo wa kulaza wagonjwa 375 kwa wakati mmoja.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment