Image
Image

News Alert:Kairuki awaondoa hofu wakazi wa Kigamboni*Asema hawataondolewa katika maeneo yao*Waliopo kwenye miundombinu muhimu watafidiwa.


Serikali imewaondoa hofu wakazi wa Kigamboni  kuwa hawataondolewa katika maeneo yao na badala yake  waliopo kwenye  maeneo ambayo miundombinu muhimu inapita watafidiwa.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi , ANJELA KAIRUKI  alipokuwa  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge

Amsema endapo wananchi hawatakuwa na mitaji wataingia ubia na wenye nayo na pale watakaposhindwa wataweza kuuza maeneo yao au watalipwa fidia.

Baadhi ya wabunge wakati wanauliza maswali ya nyongeza wameitaka Serikali kueleza ni lini Serikali itaelekeza maafisa ardhi nchini kupima maeneo ya umma ,  zikiwemo shule na hospitali , ambayo yamekuwa na migogoro ambayo wakati mwingine inaweza kusababisha uvunji f u wa amani.

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara ,Dakta   ABDALA KIGODA akijibu swali la Mbunge wa Biharamlo Magharibu , ANTHONY MBASSA ,juu ya mpango wa Serikali kudhibiti uharibifu wa miundombinu zikiwemo alama za barabarani amesema ,   katika kukabiliana na tatizo hilo Serikali imeandaa waraka wa Baraza la Mawaziri na kupendekeza kutungwa sheria itakayosimamia na kudhibiti chuma chakavu.

Na kuhusu tatizo la majengo kuporomoka ,  kutokana na madai ya vifaa vinavyotumika kutokuwa na viwango ama kujengwa chini ya kiwango ,  Waziri KIGODA amesema ili kudhibiti tatizo hilo Shirika la Viwango  Tanzania -  TBS  -  imekuwa ikihakikisha bidhaa zote zinazozalishwa nchini zinakidhi kiwango cha kimataifa cha bidhaa husika.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment