Image
Image

News Alert:Hali ya amani nchini burundi si nzuri*Kamati kukutana jumatatu kujadili na kufanya tathmini*Baraza la usalama la umoja wa mataifa laitisha kikao cha Dharua kujadili hali ya mambo burundi.


Kamati  ya  Baraza la Mawaziri la nchi za Jumiya ya Afrika Mashariki limesema hali ya amani  nchini  Burundi bado tete .
Kamati hiyo itakutana Jumatatu wiki ijayo  kufanya tathimini ya  hali itakavyoendelea kuwa nchini  humo  na  kuona   nini kifanyike,kwani mpaka sasa haijajulikani ni nani  anayeongoza nchi hiyo kati ya wanajeshi watiifu kwa Rais PIERE NKURU NZINZA na wanajeshi waluiofanya  mapinduzi .

Mwenyekiti wa mawaziri hao ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania,BERNARD MEMBE amesema ,kwa hali ilivyo hivi sasa nchini Burundi zin ahitajika jitihada za ziada kwa  kila mpenda maendeleo,ili kunusuru  vurugu zinazoendelea nchini humo .

Kuhusu mahali alipo Rais PIERE NKURUNZINZA Waziri MEMBE amekataa kutaja mahali alipo  kiongozi huyo wa Burundi.
Ingawa uchunguzi unaonyesha kuwa Rais huyo mara baada ya kuondoka na ndege jana kurudi Burundi nakushindwa kuhudhuria kikao cha EAC baada ya kupata taarifa za kupinduliwa na Jeshi hakuweza kufika baada ya kuwekewa vizuizi kufuatia amri ya Meja jenerali wa Jeshi Godefroid Niyombare kuamuru taa za uwanja wa ndege kuzimwa na kutoruhusiwa Ndege yeyote kutua nchini humo ambapo Rais Nkurunzinza Inaelezwa alirudi na yupo hapa jijini Dar es salaam na alilala moja ya hoteli kubwa mjini hapa.

Katika hatua nyingine nalo Baraza la Uslaama la Umoja wa Matiafa leo hii limeitisha kikao cha dharura kujadili hali ya mambo Burundi baada ya jenerali mwandamizi jeshini kutangaa kunyakua madaraka kutoka kwa Rais Pierre Nkurunziza. Kikao hicho cha dharura kimeitishwa na Ufaransa  huku katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon akitoa wito wa utulivu na ustahamilivu nchini Burundi. Wakati huo huo Umoja wa Mataifa unafuatilia kwa karibu kinachoendelea nchini Burundi na kusisitiza kauli ya Katibu Mkuu Ban Ki-moon aliyotoa wakati wa mkutano wa viongozi wa Muungano wa Afrika huko Addis Ababa, Ethiopia kuhusu awamu za uongozi. Hayo ni kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric aliyezungumza mjini New York, wakati wa mkutano na waandishi wa habari waliotaka kufahamu msimamo wa chombo hicho kuhusu hali iliyoripotiwa Burundi.

Jana baada ya kuenea habari Jenerali Godefroid Niyombare kumpindua Rais Pierre Nkurunziza, rais huyo alijaribu kurundi nchini kwake kutokea jijini Dar es Salamu, Tanzania alikokuwa amekwenda kushiriki kikao cha marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC.  Hata hivyo ndege yake ilishindwa kutua baada ya askari watiifu kwa Niyombare, kuzingira uwanja wa ndege wa Bujumbura. Bado haijabinika Nkurunziza yuko wapi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment