Image
Image

News Alert:Serikali yawaonya viongozi wa vyama vya siasa kuacha kutoa lugha chafu na za uchochezi wakati wa kampeni.


Serikali Wilayani Korogwe  imewaonya viongozi wa vyama vya siasa kuacha kutoa lugha chafu na   za uchochezi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu ujao wa Rais na wabunge .
Badala yake wametakiwa  watumie muda huo kutangaza sera za vyama vyao ili kuepuka viashiria vya uvunjifu wa amani katika maeneo mbali mbali wilayani humo.
Akizungumza katika kongamno la viongozi wa dini, siasa na  viongozi wa  makundi ya kimila, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe , HAFSA MTASIWA amesema mbali na wanasiasa pia amepiga marufuku wananchi kuwachangia fedha makundi ya watu wanaodai kuwa wanatoa wachawi wanaojulikana kwa jina la ''Lamba Lamba'' ambao wamekuwa wakivunja amani miongoni mwa jamii .
Kwa upande wake She ikh wa Wilaya ya Korogwe , Alhaji  ALLY ZUBEIR amewataka maimam u  wa misikiti  yote  wilayani humo   kuhakikisha wanawaeleimisha waumini wao kuhusu hali ya amani na utulivu na kuachana na mambo ya siasa katika nyumba za ibada hatua ambayo imekuwa na viashiria vya mgawanyiko baina yao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment