Serikali imewataka wananchi kuacha kutumia
mifuko ya Plastiki kuwekea au kuhifadhia chakula
kutokana na madhara yanayoweza kuwapata badala
yake watumiye vifungashio vya Glas Chuma
isiyoshika kutu na vyombo vingine vya asili.
Hayo yamesemwa Bungeni na Naibu Waziri
wa Nchi ,Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira STEPHEN MASELE
alipokuwa akijibu swali la mbunge MKIWA ADAM
KIMWANGA aliyetaka kujua serikali inachukua hatua
gani kudhibiti matumizi ya mifuk o ya
plastiki ambayo kitaalam inaonekana kuwa na madhara.
Waziri MASELE amekiri kuwa mifuko
Plastiki inaweza kusababish a madhara kwa kuweka chakula
kutokanana kemikali zilizotumika kutengeneza mifuko
hiyo kuingia kwenye chakula na kukifanya kuwa sumu.
Amesema serikali imepiga marufuku
matumizi ya mifuko hiyo yenye unene wa chini ya
Maikroni 30 na kuhamasisha matumizi ya mifuko mbadala.
Bangladesh imepitisha sheria.
Nchi ya kwanza kukataza mifuko ya rambo kutumika ni
Bangladesh kwa sheria iliyopitishwa huko mwaka 2002.. California nako
walipitisha Sheria hiyo mwaka 2012-13 na mpaka sasa hakuna sehemu utaenda
California alafu ukawekewa kitu kwenye mfuko wa rambo.
Mwaka 1992 Singapore ilipitisha sheria iliyokataza
kuuza ama kusafirisha big g kwa nchi yoyote duniani, ila big g zitengenezwe kwa
ajili ya kulika na kununuliwa na raia wa Singapore tu. Baada ya miaka 12
yalifanyika mabadiliko na kuruhusu watu wa Singapore kununua big g ambazo
hazina sukari yani Sugar-free chewing gums ambazo ni nzuri kwa meno na kinywa
cha binadamu. Kwa sasa utaratibu uliopo ukikutwa unatema big g chini au
unatafuna ovyo unapigwa faini.


0 comments:
Post a Comment