Image
Image

News Alert:TANAPA - imeshauriwa kuanzisha utaratibu wa kutoa zawadi kwa watalii wa ndani watakaofanya vizuri.


Menejmenti  ya Hifadhi za Taifa  -TANAPA- imeshauriwa kuanzisha utaratibu wa kutoa zawadi kwa watalii wa ndani,watakaofanya vizuri kwa vigezo vitakavyowekwa watakaotembelea hifadhi zake ,ukiwemo Mlima Kilimanjaro.

Rai  hiyo imetolewa na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Prof esa  FAUSTIN BEE katika kilele cha tatu cha Mlima Kilimanjaro cha Shira,katika siku ya mwisho ya kampeni ya kuwahamasisha Watanzania kupanda mlima huo.

Prof esa  BEE amesema, utaratibu huo utasaidia kuwahamasisha Watanzania ,  hasa vijana kutembelea hifadhi hizo,kutokana na idadi ndogo,ya  asilimia tano ya watalii wote waliotembelea hifadhi za taifa ambao ni Watanzania kwa miaka kumi iliyopita.

Meneja wa Benki ya CRDB tawi Marangu ,Bwana   INOCENT SILAYO amesema, ataishauri Menejment i  ya  Benki ya  CRDB kuandaa programu ya kila mwaka ya watumishi ya benki hiyo kupanda mlima huo kuwahamasisha Watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea hi fadhi hizo na kujenga afya zao.

Afisa Masoko wa KINAPA,Bwana   ANTIPUS MGUNGUS amesema, hifadhi hiyo kwa sasa inaandaa mpango wa kwenda kwenye taasisi mbali mbali vikiwemo vyuo vikuu vilivyopo Mkoani Kilimanjaro na mikoa mingine,kuwahamasisha Watanzania  kupand a mlima huo badala ya kuwaachia wageni.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment