Image
Image

News Alert:Wananchi wa Kijiji cha Longuo A Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro wanaka biliwa na tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi.



Wananchi wa Kijiji cha Longuo A Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro wanaka biliwa na tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi kutokana na kamati iliyoundwa kushughulikia kero ya maji katika kijiji hicho kujimilikishaa mradi wa maji ulioibuliwa na wananchi  kwa kuwatoza kiasi cha Shilingi Milioni 3 ili kuunganishiwa huduma ya hiyo .

Wakizungumza katika mkutano wa kijiji  wananchi hao wa me sema tatizo la maji katika kjiji hicho limedumu kwa muda mrefu na kusababisha adha kubwa kwa wananchi wa kijiji hicho kutembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi .

Kufuatia tatizo hilo wananchi hao  wameiomba Serikali  kutatua kero ya maji katika kijiji hicho  kutokana na viongozi mbalimbali  kufikia katika kijiji hicho na kuahidi kutatua tatizo la maji  bila mafanikio .

Kwa upande wake mweneykiti wa kijiiji cha Longuo A,Bwana   PAUL KISIMA amekiri kuwapo kwa tatizo hilo na kusema kuwa wananchi hao walitumia gharama kubwa kuibua mradi huo pamoja na kuchangia nguvu kazi na fedha .

Mhandisi wa maji Wilaya ya Moshi BROMEN LYIMO amesema  Serikali ya wilaya inatambua mgogoro huo na kwamba malalamiko ya wananchi hao ni ya msingi kutokana na kutozwa fedha nyingi  za kuunganishiwa huduma ya maji ambayo hayatoshelezi .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment