Image
Image

News Alert:Uchaguzi kufanyika siku za kazi Serikali yasema haijafanya utafiti kujua itapoteza nini.


Bunge limeelezwa na Serikali kuwa  haijafanya  utafiti kujua itapoteza nini  kama uchaguzi utafanyika siku za  kazi  ingawa kusimama  kwa shughuli  za  kazi huweza  kuathiri   uchumi wa nchi  kwani  siku za kazi  wafanyakazi  na  wafanyabiashara  walio wengi  huwa  wanatekeleza  majukumu  ya kikazi  ya kujipatia  kipato .
Hayo yamesemwa na  Waziri wa Nchi  Ofis i ya Waziri Mkuuu ,Sera na Uratibu wa  Bunge  JENISTA MHAGAMA alipokuwa  akijibu  swali  la  Mbunge  ASSUMPTER  MSHAMA  aliyetaka  kujua  serikali inapoteza  kitu gani  kama  itapanga   kupiga  kura  katika  uchaguzi  mkuu kufanyika  siku  za  kawaida  za  kazi .
A MESEMA  kwa   mujibu wa  Ibara  ya  74  ya katibaa  kifungu kidogo cha 6 mpaka 15   Tume  ya  Taifa ya  Uc haguzi imepewa madaraka  ya kuratibu  na kusimamia uchaguzi   ili kuwezesha  uchaguzi   ili kuwezesha uchaguzi   kufanyika  kwa mujibu  wa katiba  ya nchi.
Waziri  MHAGAMA  ameliambia Bunge kuwa Tume  ya Taif ya Uchaguzi kwa mamlaka  iliyopewa  kikatiba inaweza  ikaona  kama  ni busara  ama  itafaa  kufanya  uchaguzi  katikati  ya siku za wiki  kwani uchaguzi ni tendo la kikatiba  na matarajio  ni  kuiweka  serikali iliyochaguliw a  kwa  msingi wa haki  na sheria .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment