Serikali ya Burundi imepinga
ukosoaji wa kimataifa kuhusu rais Pierre Nkurunziza kugombea urais kwa awamu ya
tatu, na kusema kuwa uamuzi wa rais haupaswi.
"kujadiliwa".
Msemaji wa serikali ya Burundi Bw. Philippe
Nzobonariba amesema, Burundi inafuatilia shughuli za kidiplomasia zinazoendelea
ambazo zinaelekea kuharibu na kupaka matope mfumo na katiba ya nchi hiyo.
Ameongeza kuwa shughuli kuhusu mamlaka, katiba na sheria haziwezi kujadiliwa,
na hizo ni pamoja na rais Nkurunziza kugombea urais mwezi Juni, maandamano
aliyoyataja ya haramu yanayoendelea na mchakato wa uchaguzi.


0 comments:
Post a Comment