Image
Image

News Alert:Utafiti*Super Brains Media yagundua elimu inayotolewa na vyuo vya kawaida pamoja na vyuo vikuu nchini ina utamaduni wa nchi za magharibi.



Kiondo Mshana Pichani hapo -Mkurugenzi Mtendaji Super Brain Media.

                             Ijue Kampuni ya Super Brains Media.  

Kampuni ya Super Brains Media Limited ilianzishwa Januari 31,2011 kama Limited,ambayo iko Tegeta jijini Dar es Salaam,Tanzania ikiwa imesajiliwa kwa namba 81238 na kupewa TIN namba 111898642.

Baadhi ya malengo yaliyo sababisha kampuni hii kuanzishwa ni haya yafuatayo.
·        Kuanzisha na kuendesha vyuo vya habari vyenye ubora mkubwa vinavyofundisha Uandishi wa Habari kwa vitendo hadi ngazi ya chuo kikuu.

·        Kufanya biashara ya kuchapisha Magazeti,Kutoa ushauri wa kitaalamu na kuendesha Semina,Washa,Kongamano,Kozi fupi,Kozi ndefu na kutoa elimu kwa wanafunzi wa vyuo hivyo.

·        Kuandika,kuhariri na kuchapisha magazeti,majarida,vitabu,daftari pamoja na kufanya kazi za utafiti.

·        Aidha kampuni hii ilianzishwa baada ya kufanya utafiti na kubaini kuwa elimu inayotolewa kwa wanahabari hapa nchini,ina pengo kubwa katika ufundishaji wa masomo ya uandishi wa habari,ambalo lilihitaji kuzibwa.

1.     Mapengo yaliyoonekana ni kwamba:

Vyuo vingi vya Habari nchini vimekosa elimu ya vitendo katika masomo yanayo tolewa ambayo ndiyo muhimu kwa vijana chipukizi katika tasnia ya habari nchini.

2.     Utafiti uliofanywa na kampuni hii umegundua kuwa elimu inayotolewa na vyuo vya kawaida pamoja na vyuo vikuu  nchini ina utamaduni wa nchi za magharibi.

§  Kwa mfano,walimu asilimia kubwa wanaofundisha vyuo hivyo wana elimu ya kimagharibi,Vitabu walivyosoma ni vya magharibi kwa hiyo hata dhana wanayo irithisha kwa wanafunzi ni ya kimagharibi ambayo haifanani wala hai saidii katika mazingira ya kiafrika.

·        3.Vijana wanao maliza vyuo na kuajiriwa moja kwa moja katika vyumba vya habari wanashindwa kuiweka nadharia waliofundishwa katika vitendo kutokana na ukweli kwamba siku hizi wahariri hawana muda wa kuwaelekeza kuhusu utendaji wa kazi zao katika vyumba vya habari au kuwapa mafunzo kazini kama ilivyokuwa zamani.

·        Kutokana na matatizo haya ya kukosa maelekezo,vijana wengi wapya wenye uwezo wanapoajiriwa husindwa kuakabili mazingira ya vyumba vya habari,hatimaye huchanganyikiwa na kukimbia taaluma ya uandishi wa habari.

·        Ili kuziba pengo hili kampuni ya Super Brains Media LTD (SBM), kwa kuanzia imeanzisha chuo cha Uandishi wa habari kwa vitendo kijulikanacho kama Practical School of Journalism(PSJ) ambacho kimeshasajiliwa na serikali.

·         Pia kampuni imeanzisha gazeti la uchunguzi lijulikanalo kama Wajibika ambalo tayari limeshasajiliwa na serikali na linapatikana mikoa yote nchini Tanzania.

·        Hata hivyo ili kukamilisha mafunzo ya habari kwa vitendo,kampuni imejitahidi kuwa na studio za radio na Television ambazo kwa sasa zinapatikana Online kwa majina ya SBM Radio na SBM Tv,pamoja na Blog.

·        Kwa wale wote watakao taka kutembelea Blog yetu,inaitwa SBM Broadcast na kuipata kwake unatakiwa uandike www.sbm broadcast.blogsport.com ambayo hadi sasa ina jumla ya watu 32,879.->>http://sbmbroadcast.blogspot.com

·        Kutokana na wingi huu wa watu wanao tembelea Blog yetu. Super Brains Media inawakaribisha wote kutangaza biashara na matukio mbali mbali katika sbm broadcast pamoja na gazeti la Wajibika.


¨     Kiondo Mshana.

¨     Mkurugenzi Mtendaji.

¨     Super Brain Media.

Simu:  +255715333186

       Au +22767333186

Ofisini:+255 737 227 610

Baruapepe:superbrains2014@gmail.com
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment