Makamu wa rais wa shirikisho hilo Jeffrrey
Webb ni kati ya waliokamatwa kwa kosa la kupokea rushwa pamoja na viongozi
wengine wa juu 6.
Uchunguzi mwingine umeshaanza kufanyawa
kuhusu namna nchi zitakazokuwa wenyeji wa kombe la dunia kwa mwaka 2018 na 2022
zilivyopewa heshima hiyo.
Lakini Fifa imesisitiza kuwa urus na Qatar
ndio wenyeji wa kombe ladunia kwa mwaka 2018 na 2022 kwani wanaamini uchunguzi
huo hautabaini baya lolote.
Na timu ya mpira wa kikapu ya Cleveland Cavaliiers
imetinga fainali za ligi ya mpira wa kikapu ya marekani baada ya kuwachakaza Atlanta
Hawks kwa vikapu 118-88.
Kwa mara nyingine tena Lebron James
aliibeba Cavs akimaliza na vikapu 23 kuokoa mipira mara 9 na kutoa pasi za
mwisho 7 na kisha kuwa mshangiliaji mkuu kwa karibu robo nzima ya mwisho ya
mchezo.
Cavalliers sasa wanasubiri mshindi kati ya
Golden State Warriors na Houston Rockets.



0 comments:
Post a Comment