Waziri mkuu huyo amekutana na jaribio hilo la
kumuua wakati yeye na msafara wake
wakitokea katika mkutano wa bunge kwenye mji wa Tobruk.
Waziri mkuu -Al Thinni anatambulika na jumuiya za
kimataifa kama kiongozi halali wa libya ingawa anaongoza baadhi ya maeneo
katika nchi hiyo.
Hali hiyo inatokana na mji mkuu nchi hiyo kuwa chini
ya usimamizi wa wapiganaji wa jihadi ambao wanadaia na wao wanaongoza serikali
iitwayo serikali mbadala.


0 comments:
Post a Comment