Wananchi na wanachama wa CHADEMA wakimsikiliza kwa makini mlezi wa Bawacha Bi,Liliani Wasira wakati akizungumza nao juu ya kujitokeza wakati wa mchakato wa zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura Jijini Dar es Salaam.
Dar es Salaam.
Baraza la wanawake wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema jimbo la Segerea jijini Dar-es-Salaam wamesema wanakusudia kuanza kutembea nyumba kwa nyumba kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwa wingi katika daftari la wapiga kura.
Hayo yameelezwa na mlezi wa Bawacha Bi,Liliani Wasira
ambapo amesema lengo la kufanya hivyo ni ili wananchi wawe na utayari ili zoezi hilo litakapofika mkoani Dar-es-Salaam
waweze kupiga kura.
Hata hivyo katika zoezi hilo amewaasa akina mama
kuto kurudi nyuma na kujiona hawawezi kufanya kazi kama wanavyuo fanya wanaume
na kuwataka wasiwe waoga wajitokeze ili kuweza kugombea katika uongozi wa juu
hususa Udiwani,Ubunge, na hata Urais kwani wanaweza.
0 comments:
Post a Comment