Image
Image

Waziri mkuu wa zamani wa Uganda assema atagombea nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.


Waziri mkuu wa zamani wa Uganda Amama Mbabazi ametangaza kuwa, atagombea nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka ujao nchini humo.
Mbabazi ameibuka kuwa mpinzani mkubwa dhidi ya rais wa sasa wa Uganda Yower Museveni, ambaye alifanya naye kazi kwa zaidi ya miaka 40. Rais Museveni alimfukuza kazi Mbabazi mwaka jana baada ya ripoti kutoka chama cha NRM kuwa waziri mkuu huyo anawania nafasi ya juu zaidi ya uongozi nchini humo. Mbabazi pia alifutwa wadhifa wa katibu mkuu wa chama hicho.
Uchaguzi mkuu utafanyika mwezi Februari mwaka ujao nchini Uganda, huku wabunge wa chama tawala cha NRM tayari wamemchagua rais Museven kugombea tena nafasi hiyo akiwa mgombea pekee wa urais.
Rais Museveni ameshika madaraka hayo tangu mwaka 1986.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment