Image
Image

Naibu mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kijeshi ya China afanya ziara nchini Marekani.


Naibu mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kijeshi ya China Bw. Fan Changlong amefanya ziara nchini Marekani kuanzia tarehe 8 hadi 12 mwezi huu. Akiwa nchini humo, Fan alifanya mazungumzo na waziri wa ulinzi wa Marekani Ashton Carter, na kushuhudia kusainiwa kwa Waraka wa mfumo kuhusu mawasiliano na mazungumzo kati ya majeshi ya nchi kavu ya China na Marekani.
Fan Changlong amesema, rais Xi Jinping wa China atafanya ziara nchini Marekani mwezi Septemba mwaka huu, na hili ni jambo muhimu katika uhusiano kati ya nchi hizo mbili kwa mwaka huu. Ameongeza kuwa ziara yake hiyo inalenga kutimiza maoni muhimu ya pamoja ya viongozi wa nchi hizo mbili na kuhimiza uhusiano kati ya majeshi ya China na Marekani uendelezwe kwa utulivu. Kuhusu suala la Bahari ya Kusini ya China, Fan Changlong ameihimiza Marekani iendelee na msimamo wa kutounga mkono upande wowote, kupunguza shughuli za kijeshi kwenye eneo la Bahari hiyo, kushughulikia masuala kwa haki, na kutofanya mambo yanayoharibu uhusiano kati ya majeshi ya nchi hizo mbili na kuathiri amani na utulivu wa kikanda.
Kwa upande wake, Carter amesema suala la Bahari ya Kusini ya China si suala lililopo kati ya China na Marekani, na Marekani haitaunga mkono upande wowote kwenye mvutano wa mamlaka ya Bahari hiyo, vilevile imezitaka pande husika zifanye mazungumzo ili kutatua suala hilo kwa njia ya amani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment