Dakika mbili baadaye nahodha wa timu ya England Wayne Rooney aliweza kuipatia timu yake ushindi kwa kupachika bao katika dakika ya 86.
England imezidi kuongoza kundi E lenye timu za Estonia, San Marino, Lithuania, Switzerland na Slovenia.
Baadhi ya michezo iliyochezwa Jumapili ni pamoja na ule kati ya Sweden na Montenegro ambapo Sweeden iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.
Hispania ilichomoza na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Belarus. Austria iliicharaza Urusi bao 1-0, nayo Uswisi ikiibwaga Lithuania kwa mabao 2-1 na Ukraine ikiigaragaza Luxembourg mabao 3-0.
Katika michezo ya Jumamosi Ujerumani iliifanyia mauaji Gilbratar kwa kuitandika magoli 7-0 nayo Poland ikiilaza Georgia mabao 4-0 huku Scotland na Jamhuri ya Ireland zitoka sare ya bao 1-1.
0 comments:
Post a Comment