Kindumbwendumbwe kwa mataifa ya Afrika kufuzu
kucheza fainali za Afcon mwaka 2017 kimeanza kwa michezo kadha kuchezwa
mwishoni mwa wiki. Ghana ilikuwa na
kazi nyepesi baada ya kuirarua Mauritius magoli 7-1. Asamoah Gyan na
Jordan Ayew wote walifunga mara mbili wakati Ghana ikiilaza Mauritius kwa mabao
7-1.Ghana ilifungwa
na Ivory Coast kwa penalti katika fainali za mwaka huu, lakini sasa inaonekana
kupania kucheza fainali za mwaka 2017.Mchezo huo wa kundi H ulichezwa mjini
Accra, Jumapili. Ghana iliwazidi
kwa ubora Mauritius ambayo imewahi kucheza mara moja katika historia ya
michuano hiyo ikiwa ni mwaka 1974. Nayo Nigeria
ikiikaribisha Chad mjini Kaduna iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, huku
Afrika Kusini ikishindwa kuutumia vema uwanja wao baada ya kutoka suluhu ya 0-0
na Gambia.
Kwa timu za
Afrika Mashariki Uganda ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Botswana, Rwanda
ikiilaza Msumbiji bao 1-0, huku Kenya ikitoka sare ya bao 1-1 na Congo. Burundi
imecharazwa na Senegal mabao 3-1, nayo Tanzania ikiambulia kipigo cha mabao 3-0
kutoka kwa Misri.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment