Image
Image

Tamwa yaungana na mataifa kuadhimisha siku ya mtoto Afrika.

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kinaungana na mataifa yote ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike kikiitaka jamii ya Tanzania na Afrika kwa ujumla kupinga ndoa za umri mdogo kwani ni vitendo vinavyokiuka haki za binadamu na pia havishughulikiwi kwa kiwango stahiki.
Siku ya Mtoto wa Kike ambayo kauli yake mbiu mwaka huu ni “Miaka 25 Baada ya Kupitishwa kwa Mkataba wa Haki za Mtoto wa Afrika: Kuongeza Kasi na Jitihada Zetu za Pamoja Kutokomeza Ndoa za Utotoni Afrika”  kwani ni ukiukwaji wa haki za mtoto wa kike kutokana na kuwa ndoa nyingi zinapangwa na kujikita zaidi katika makubaliano kati ya anayetaka kuoa na wazazi wa mtoto wa kike na kushindwa kuhakikisha mhusika mkuu anaridhika.
Ndoa za umri mdogo zimeonyesha kuongezeka kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita ambapo takwimu zinaonyesha kuwa bara la Afrika na Asia vitendo hivyo vinaongoza.
Kwa mujibu wa Utafiti wa Watu na Afya  nchini Tanzania (TDHS) wa mwaka 2010, wastani wa watoto 4 katika kila watoto 10 wa kike wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18 na inakadiriwa kuwa asilimia 37 ya wanawake wa umri kati ya miaka 20 na 24 kwa mwaka 2000 – 2011 waliolewa au kuwa na mahusiano ya ndoa walipofikia umri wa miaka 18. 
Aidha kwa mikoa ya Tanzania imeonyesha kuwa ndoa za umri mdogo zinaogoza katika mikoa ya Shinyanga (59%), Tabora (58%), Mara (55%) na Dodoma (51%) ambapo kisiwani Pemba imeonyesha kuwa katika kila watoto 10 wanaokwenda shule, watano hawamalizi masomo yao kutokana na kuolewa.
Sababu za kuendelea kwa ndoa za utotni nchini Tanzania ni Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 ambayo inaruhusu watoto wa kike wenye umri wa miaka 14 kuolewa kwa ruhusa ya mahakama, na wenye umri wa miaka 15 kuolewa kwa ridhaa ya wazazi wao, sheria za kimila za baadhi ya makabila kutoa maamuzi ya ndoa kulingana na mila na desturi zao.
Aidha sababu zingine ni ndoa za umri mdogo kujitokeza zaidi katika maeneo yenye familia masikini, mila na desturi kandamizi ambapo kwa utafiti wa Utu wa Mtoto wa Kike ( Child Dignity Forum- CDF), watoto wa kike wanaotoka kwenye kaya masikini wana uwezekano wa kuolewa mara mbili zaidi kabla ya umri wa miaka 18 ikilinganishwa na kaya zenye uwezo
TAMWA inaamini kuwa wadau mbalimbali hapa nchini na duniani wakishawishi hatua za kushughulikia mahitaji ya watoto hasa wa kike kwa kuelekeza nguvu kwa wahusika wote pamoja na kuondoa vikwazo vyote vinavyozuia kufikiwa kwa haki hizo, ndoa hizo zitapungua kama siyo kuisha kabisa.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment