Image
Image

Breaking News:Mbunge wa jimbo la Ukonga afariki dunia Dodoma.


Mbunge wa jimbo la ukonga  liliopo jijini Dar es Salaam kwa kupitia chama cha mapinduzi ccm Mh. Eugean Mwaiposa amefariki dunia leo asubuhi majira ya saa nne nyumbani kwake mjini Dodoma, Bunge la bajeti limeahirishwa hadi alhamisi.
Akitangaza taarifa ya kifo hicho leo Bungeni mjini Dodoma katiak bunge la bajeti linaloendelea naibu Spika Job Ndugai amesmea marehemu mwaiposa alikuwa anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la Damua ambalo ndilo limesababisha kifo chake
Kutokana na msibo huo Bunge la bajeti limeahirishwa hadi alhamisi ambapo kesho mbunge huyo ataagwa mjini Dodoma na kusafirishwa kuletwa jijini Dar es Salaam kwa mipango mingine ya mazishi.
Kwa upande wa Baadhi   ya  wabunge wamesema  taarifa  hizo  za  msiba  huo wamezipokea  kwa masikitiko  makubwa  kwa  kuwa  mpaka  jana  jioni  kabla  ya  kifo  chake  walikuwa  naye   Bungeni   lakini leo hawapo naye tena.
Awali  kabla  taarifa  za  msiba  huo waziri wa afya na  ustawi  wa  jamii  akiwasilisha Bajeti  ya  wizara yake  amesema  sekta  ya  afya  inakabiliwa  na changamoto  ya upungufu   wa  wawatumishi   kwa  asilimia  58 .
Nao watu wa sekta  ya afya  wamesema  serikali   bado  haijaweka  msisitizo mkubwa  katika  utafiti  wa  dawa  mbalimbali  ili kukabiliana  na tatizo  la  upungufu wa dawa  kwani  baadhi  ya  dawa  zilizopo  sasa  hivi  zingine  zinaonekana  kushindwa kufanya  kazi na hivyo kunatakiwa  dawa  mbadala.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment