Image
Image

Chadema yalalamikia kasi ndogo ya uandikishaji wapiga kura Mwanza.


Naibu katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Zanzibar SALUM MWALIM amefanya ziara ya kutembelea vituo vya kujiandikishia wapiga kura katika wilaya za ilemela na nyamagana mkoani Mwanza na kushuhudia kasi ndogo ya uandikishaji na uchache wa mashine za kielektroniki  zisizoendana na idadi kubwa ya wananchi wanaojitokeza kujiandikisha.
Kufuatia hali hiyo,naibu katibu mkuu wa chadema Zanzibar SALUM MWALIM ameonyesha wasiwasi wa kutofanikiwa kwa zoezi hilo katika baadhi ya vituo alivyovitembelea kutokana na wananchi kutumia zaidi ya siku tatu vituoni bila kuandikishwa na kusababisha baadhi yao kuanza kukata tamaa, huku mizengwe, upendeleo na vitendo vya rushwa vikidaiwa kutawala zozi hilo lililoanza juni 9 mwaka huu katika baadhi ya kata za wilaya ya ilemela na nyamagana.
Baadhi ya wananchi waliokutwa katika vituo vya kuandikishia wapiga kura vya kata za ilemela, sangabuye, mkolani na buhongwa ambavyo naibu katibu mkuu huyo wa chadema Zanzibar amevitembelea akiwa ameongozana na waandishi wa habari, wamewalalamikia baadhi ya waandikishaji wasaidizi kwa kushindwa kutumia barabara mashine za BVR na kwa hali hiyo kujikuta wakitumia muda mrefu kuandikisha watu wachache.

Baada ya naibu katibu mkuu huyo kusikiliza kilio cha wakazi wa mkoa wa Mwanza ambao wanaendelea kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya kujiandikishia ili kuhakikisha wanapata haki yao ya kikatiba ya kuwachagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi mkuu ujao, nini ushauri wa naibu katibumkuu wa chadema Zanzibar kwa watendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment