Image
Image

China yatoa wito wa kudumisha mafanikio yaliyopatikana katika mapambano dhidi ya Ebola.


Naibu balozi wa China katika Umoja wa Mataifa Bw. Wang Min amesema, mafanikio yaliyopatikana katika mapambano dhidi ya Ebola bado si ya kuridhisha na jumuiya ya kimatiafa inatakiwa kuwa makini na kufanya jitahida ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.
Wang amesema hayo katika mkutano usio rasmi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Ebola.
Amesema, kazi muhimu zaidi kwa sasa ni kusaidia nchi zinazoathiriwa na ugonjwa huo kurejesha uchumi wao, kuimarisha mfumo wa afya ya umma, na kuanza ushirikiano katika udhibiti wa magonjwa, utoaji wa mafunzo na utafiti wa dawa. Amesema, China inajadiliana na nchi husika na Umoja wa Afrika kuhusu mpango wa kuanzisha "kituo cha kudhibiti na kuzuia ugonjwa cha Afrika".
Pia China imechangia dola za marekani milioni 6 kwa mfuko wa kupambana na Ebola wa Umoja wa Mataifa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment