Image
Image

Kenya: yaadhimisha miaka 52 ya uhuru wake.


Kenya inaadhimisha miaka 52 ya Madaraka kukumbuka siku ambayo wakoloni Waingereza mwaka 1963 walitangaza kuwa nchi hiyo itaanza kujitawala.
Siku hii pia inatumiwa kuwakumbuka wakenya waliopigania uhuru wa nchini hiyo miaka ya hamsini na sitini kabla ya kujinyakulia uhuru chini ya vuguvugu la Mau Mau.
Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kulihotubia taifa katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi.
Maadhimisho ya mwaka huu yanakuja wakati nchini hiyo ikikabiliana na changamoto za usalama kutokana na vitisho vya kundi la wanamgambo wa kiislamu la Al Shabab kutoka nchini Somalia.
Hivi karibuni kulitokea makabiliano makali kati ya vyombo vya usalama na wanamgambo wa Al Shabab. Makabiliano hayo yalitokea Jumatatu usiku Mei 25 , Kaskazini Magharibi mwa Kenya. Kijiji cha Yumbis na maeneo mengine yaliyopembezoni katika Kaunti ya Garissa, yamekua yakilengwa na wanamgambo hao wa Al Shabab.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment