Image
Image

LIPUMBA:kama taifa lina nia ya dhati ya kulinda amani,haina budi kusimamia haki ya makundi yanayoishi kwa wasiwasi.


Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi-UKAWA Profesa IBRAHIMU HARUNA LIPUMBA amesema, kama taifa lina nia ya dhati ya kulinda amani, haina budi kusimamia haki ya makundi yanayoishi kwa wasiwasi kama walemavu wa ngozi na vikongwe.
Profesa LIPUMBA ametoa rai hiyo wakati akiwahutubia wananchi mjini Tabora, akiwa katika ziara ya kuwahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,
Akizungumzia changamoto zinazowakabili walemavu wa ngozi albino na kuishi bila amani katika nchi yao, amesema serikali haijatoa msimamo wa kuwanusuru na janga la kuwindwa kama wanyama.
Wakizungumzia changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa wa Tabora baadhi ya viongozi waandamizi wa Chama cha Wananchi mkoani humo wamesema mabadiliko ya wananchi wa tabora yataletwa na wakazi wa Tabora wenyewe kwa kufanya uamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu ujao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment