Mashindano hayo ambayo huyakutanisha makundi mawili
hasimu ya Wagika na Wagalu yamefanyika kwenye viwanja ya CCM na
halimashauri ya mji wilayani Bariadi na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi kutoka
maeneo mbalimbali ya mkoa huo.
Wakiongea mara baada ya kumalizika kwa ngoma hiyo
baadhi ya wananchi waliohudhulia ngoma hiyo wamewahimiza wanananchi wa mkoa huo
kuendelea kuuenzi utamaduni wa mila za kisukuma kwa faida ya vizazi
vijavyo.
Wananchi hao wamesema utamaduni huo hauna budi
kuenziwa kwani ndiyo njia pekee ya kuwakutanisha wasukuma na kubadilishana
mawazo kwa njia ya ngoma huku wakitafakali namna ya kuanza msimu mpya wa kilimo
Katika tamasha hilo hilo kundi la Wagika limeibuka
mshindi kwa kuwashinda wenzao wagaru na kupewa zawadi mbalimbali zikiwemo fedha
na Ng’ombe.


0 comments:
Post a Comment