Image
Image

Kikundi cha Boko haram kimeua watu 15 Nigeria..


Watu 15 wameuawa nchini Nigeria wakati wapiganaji wa kikundi cha Boko Haram waliposhambulia kijiji kimoja cha mbali Kaskazini-Mashariki mwa nchi hiyo.
Wakazi wa kijiji cha Huyum, Wilaya ya Askira-Uba, Jimbo la Borno ambacho wiki za  hivi karibuni kimekumbwa na mashambulio wanasema k atika shambulio hilo wapiganaji  walifyatua risasi ovyo na kuchoma moto mamia ya nyumba.
Mmoja wa wakazi hao aliyekimbilia jimbo jir ani la Amadawa amesema wavamizi  waizunguka kijiji hicho na kufyatua risasi na n dani ya kijiji ambako walimwaga  mafuta kwenye nyumba 500 za udongo zilizoezekwa nyasi na kuzichoma m o to.
Shambulio hilo lilikuja wakati wakuu wa majesh i kutoka Nigeria na nchi jirani  wakikutana kuandaa mipango ya kukiangamiza kikundi h icho ambacho katika mashambulio  yake katika miaka sita iliyopita kimeua zaidi ya watu 15,000.
Mipango hiyo ya wakuu wa majeshi itajadiliwa kesho na viongoz i Nigeria, Cameroon, Niger na Chad na kwa mara ya kwanza rais wa Beni n naye pia amealikwa kuhudhuria  kikao hicho chenye nia ya kuanzisha kikosi cha pamoja kuangamiza kikundi hicho.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment