Image
Image

KIU Yaiomba kamati ya bunge kuwasikiliza na kutatua kero zinazowakabili chuoni hapo.


Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala jijini Dar es Salaam wameiomba kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za jamii kwenda chuoni hapo ili kuwasikiliza na kutatua kero zinazowakabili wanafunzi wanaosoma chuoni hapo.
Ombi hilo limekuja baada ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi DR. SHUKURU KAWAMBWA kudaiwa kushindwa kuutatua mgogoro huo huku wanafunzi hao wakipata mateso makubwa.
Aidha baadhi ya wanafunzi hao wamekwenda mbali zaidi kutoa madai ya kutambuliwa kama wanafunzi kutoka nje ya nchi huku serikali ikitambua kuwa si kweli kutokana na kupata mikopo ya elimu ya juu kama wanafunzi wengine wazawa wanavyopata lakini pia wakataka ufafanuzi wa baadhi ya masuala kutoka serikalini.
Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala cha jijini Dar es salaam kimekuwa kikikumbwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya chuo hicho na wanafunzi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment