Image
Image

News Alert:Vyama vya waongoza watalii na wapagazi watangaza mgomo usio na kikomo nchi nzima ikiwa hawatalipwa stahiki zao.


Vyama vya waongoza watalii na wapagazi nchini vimesema vitafanya mgomo wa nchi nzima  usio na kikomo ifikapo tarehe 30 mwezi huu kama serikali haitatoa majibu sahihi juu ya malalamiko yao  ya kuongezwa viwango vya malipo ya kazi zao ambazo wanazifanya katika mazingira magumu na hatarishi kwa maisha yao.
Tamko hilo limetolewa na mkutano mkuu maalum uliyoshirikishwa vyama tisa kutoka kanda zote   kufuatia hatua ya makampuni ya mawakala wa utalii nchini kupuuza maagizo ya Wizara ya Mali asili na Utalii mwaka  2009 kuongeza viwango na kuyafanya makampuni hayo kulipa wastani wa dola tano hadi 10.

Mwenyekiti wa Chama cha Waongoza Watalii Mkoani Kilimanjaro Bwana RESPICIUS BAITWA amesema  makampuni hayo yamepuuza kulipa kwa siku viwango hivyo vya wastani wa dola 10, 15  hadi 20 kwa wapagazi, wapishi na waongoza watalii kwa siku.

Naye Katibu wa  Muungano wa Vyama  vya  Wapagazi nchini Bwana  MUGABO MAGOTO ameitupia lawama  serikali kwa kutoyachukulia hatua za kisheria baadhi ya makampuni ya uwakala wa utalii yanayofanya biashara hiyo bila kibali na kuliibia taifa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment