Image
Image

Mwanamke atupa mtoto chooni wilayani hai*Jeshi la polisi linamshikilia kwa tuhuma za kutupa kichanga hicho.


Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina moja la DAINESS maarufu kama MANKA ambaye ni mkazi wa Mambo ya Raha, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro anahojiwa na polisi kwa tuhuma za kujifungua na kutupa chooni kitoto kichanga.
Kitoto hicho kichanga cha kiume kinachokadiriwa kuwa na miezi tisa kilitupwa chooni nyumbani kwa jirani ambaye ni mchungaji wa kanisa la Pentekoste.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanamke huyo ambaye ni mama mwenye watoto wawili amebainika kufanya kitendo hicho nyakati za usiku baada ya mwenyewe kuanza kueleza watu kwamba kuna mwanamke aliyetupa chooni kitoto kichanga kilichosikika kikilia usiku kucha.
Polisi walipokagua chooni walibaini kuwepo kwa kichanga hicho kilichokuwa kimefungwa kwenye mifuko ya nailoni,maarufu kama Rambo,huku Kikiwa tayari kimekufa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment