Image
Image

Tume ya Taifa ya Uchaguzi yaeleza sababu za kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi katika baadhi ya maeneo.


Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeeleza sababu za mashine za kielektroniki maarufu kama BVR kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi katika baadhi ya maeneo kwamba kumesababishwa na hali ya hewa na sio tatizo la mashine.
Ofisa wa Idara ya Daftari la Wapiga Kura katika tume hiyo Bwana JAMBIA KOBELSK amesema mashine hizo ambazo ni mpya zinafanya kazi kwa ufanisi lakini kuna baadhi ya maeneo zinachagua hali ya hewa.
Hali hiyo inasababisha zoezi hilo kwenda taratibu hatua ambayo imeanza kufanyiwa kazi ili azma iliyowekwa ya kukamilisha mchakato huo iweze kufikiwa.

Awali Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Bwana SALIM CHIMA amewataka waandikishaji kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi kwa sababu endapo watafanya zoezi hilo pasipo kuzingatia kanuni wanaweza kusababisha machafuko katika uchaguzi uchaguzi mkuu ujao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa zoezi hilo mkoni Tanga Bwana LEWIS KALINJUNA amesema kikubwa zaidi ni jinsi gani ya kujifunza matumizi ya mashine za kielektroniki ili kurahisisha zoezi hilo liweze kufanywa kwa ufanisi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment